Matumizi Kumi ya Nukta (.)

Nukta (.) ni alama muhimu ya uakifishaji katika Kiswahili. Hutumika kwa njia mbalimbali kama ifuatavyo:

  1. Kuonyesha mwisho wa sentensi
    Mfano:
    Watoto wamerudi nyumbani.
  2. Baada ya vifupisho vya maneno
    Mfano:
    Bw. Otieno atakuja leo.
    Bi. Asha ni mwalimu.
  3. Katika vifupisho vya vyeo au taaluma
    Mfano:
    Dkt. Kamau ni daktari bingwa.
    Prof. Wanjiku anafundisha chuo kikuu.
  4. Kuonyesha sehemu ya desimali katika hesabu
    Mfano:
    Mtoto ana miaka 6.5.
    Alipata alama 72.5.
  5. Kuandika fedha zenye senti
    Mfano:
    Bei ya sukari ni sh. 120.50.
  6. Kuonyesha saa na dakika kwa mfumo wa desimali
    Mfano:
    Mkutano utaanza saa 10.30 asubuhi.
  7. Katika vifupisho vya majina ya taasisi
    Mfano:
    U.N.O. ni shirika la kimataifa.
    K.C.S.E. ni mtihani wa kitaifa.
  8. Katika herufi za mwanzo za majina (initials)
    Mfano:
    J.K. Mwangi alihudhuria sherehe.
  9. Kuonyesha mwisho wa wazo katika maandishi mafupi
    Mfano:
    Kazi imekamilika.
  10. Katika takwimu za kisayansi au kihisabati
    Mfano:
    Umbali ulikuwa kilomita 3.75.

Usambamba katika fasihi

Usambamba ni urudiaji wa sentensi zenye miundo sawa katika fasihi au mishororo yenye mpangilio unaofanana katika shairi. Hii huleta mtiririko mzuri, urari wa mawazo, na msisitizo wa ujumbe unaotolewa.

Sifa za Usambamba:

  1. Mishororo hufuatana katika aya moja au ubeti mmoja

Katika shairi, usambamba hutokea pale ambapo mistari miwili au zaidi ina mpangilio sawa na hufuatana katika ubeti mmoja.

  1. Huweza kutumia miundo sawa ya maneno

Sentensi au mishororo hutumia maneno yanayofanana katika muundo, kama vile vitenzi, majina, au vivumishi, ili kuleta urari wa kisanaa.

  1. Huongeza msisitizo na ufanisi wa ujumbe

Kwa kurudia miundo sawa, msomaji au msikilizaji hupata urahisi wa kuelewa wazo kuu na kulikumbuka kwa wepesi.

  1. Huongeza urembo wa lugha na mtiririko mzuri wa maneno

Usambamba hutumika katika mashairi na hotuba ili kuyafanya yawe na mvuto wa kifasihi.

Mfano wa aya yenye Usambamba

Maisha ni safari yenye changamoto na mafanikio. Tunazaliwa tukiwa dhaifu, tunakua tukiwa na matumaini, tunazeeka tukiwa na hekima. Katika safari hii, tunajifunza kutoka kwa makosa, tunakua kutokana na uzoefu, tunafaulu kwa juhudi zetu. Kila siku mpya ni nafasi mpya; tunapanga malengo, tunafanya kazi, tunatimiza ndoto zetu. Wakati mwingine tunakumbana na vikwazo, lakini tunavumilia majaribu, tunajifunza kutoka kwa matatizo, tunainuka baada ya kuanguka. Hivyo ndivyo maisha yalivyo; tunapenda, tunasaidia, tunajenga jamii bora.

Mfano katika Shairi
Njia ya Maisha

Tunapanda mlima, tunashuka bondeni,
Tunatafuta njia, tunapambana nayo.

Tunahangaika leo, tunapumzika kesho,

Tunapanda mbegu, tunavuna mavuno.

Tunavuka mito, tunavuka mabonde,

Tunashinda dhoruba, tunafurahia jua.
Tunatafuta kweli, tunakataa uongo,

Tunapenda haki, tunapinga dhuluma.

Tunapiga hatua, tunafika mbali,

Tunajifunza leo, tunatumia kesho.

Tunashinda giza, tunakumbatia mwanga,

Tunapenda amani, tunachukia vita.

Alama za uakifishaji

Alama za uakifishaji hutumika katika maandishi ili kufafanua maana, kutenganisha mawazo, na kupanga sentensi. Zinasaidia wasomi kuelewa jinsi sentensi inavyopaswa kusomwa, kama ni swali, taarifa, au mshangao, na kutoa mapumziko au msisitizo inapohitajika. Baadhi ya alama za uakifishaji zinazotumiwa sana ni kama vile:

  1. Nukta (.)
  2. Koma (,)
  3. Kiulizi(?)
  4. Alama ya mshangao (!)
  5. Koloni (:)
  6. semikoloni (;)
  7. Alama za kunukuu (“ ”)
  8. kibainishi (’)
  9. Mabano ( )
  10. kistari kifupi (-)
  11. alama za dukuku (…)

Alama za uakifishaji zinasaidia kupanga maandishi na kuhakikisha kwamba maana inayokusudiwa inafikishwa wazi kwa msomi/msikilizaji.

Alama za mtajo/usemi (” ”)

a) Usemi Halisi
“Njoo kesho,” mama akamwambia.

b) Lugha Geni/Neno la Kukopwa

“Ninunulie ‘Indomie’ ukifikia sokoni.

c) Kuandika Anwani za Filamu,

“Vioja Mahakamani”


Nukta za Dukuduku (…):

a) Kuonyesha maneno yameachwa
Haraka haraka…

b) Kukatizwa usemi/kauli

Mama: Umesema…

Mtoto: Nimesema nitarudi jioni.


Koma/Mkato/Kipumuo (,):

a) Pumziko fupi katika sentensi
Je, utarudi leo?

b) Kuorodhesha
Alinunua mboga, samaki, nyanya, na viazi.


c)Katika Usemi Halisi

“Nitachelewa,” mama akamwambia.

d) Kuandika Anwani

Wizara ya Elimu,
S.L.P 10,
Naoirobi.

e) Kuandika Tarehe

Alibatizwa mwezi wa Julai, tarehe 20, 2007.


Ritifaa/Kibainishi (’):

a)Herufi imeachwa
Wal’otutuma

b)Shadda/Mkazo

‘iba, ka’lamu


c) Sauti ya King’ong’o

Ng`ombe amekufa.


Mshazari/Mkwaju (/):

a) Tarehe
Alizaliwa tarehe 5/6/1998.

b) Kuonyesha Kumbukumbu
KUMB 1/2024

c) Kuonyesha Visawe
Nenda katika shule/skuli.

d) Kuonyesha “Au”
Wazazi/walezi wamearikwa.


Kistari kifupi (-):

a)Kuandika Tarehe
5-6-2013

b)Kutenga Silabi
a-la-ye

c) Hadi/Kipindi cha Tukio Fulani
1999-2008

d) Kutenganisha Usemi na Msemaji
Lazima tufanye kazi kwa bidii-Kibaki


Kistari Kirefu (–):

a) Kutoa Maelezo Zaidi
Nchi za Afrika Mashariki – Kenyana Tanzania – zinatumia Kiswahili kama lugha ya kitaifa.

c) Kuonyesha Msemaji wa Kauli Fulani
Umoja ni nguvu – Nyerere.


Kikomo/Kitone/Nukta (.):

a) Mwisho wa Sentensi
Atafika kesho.

b) Kuandika Tarehe
12.5.2021

Kuonyesha Ufupisho wa Maneno
Dkt., Bw.,

Kutenga Shilingi na Senti
10.20 – Shilingi kumi na senti ishirini


Nusu/Semi Koloni/Nukta Mkato (;):

a) Kugawa Sentensi Bila Viunganishi
Amekulete zawadi nyingi; hazijakufurahisha.

Kama Kipumziko Katika Sentensi Ndefu
Baada ya kuchunguza hati aliyopewa na wafanyabiashara hao, aligundua haikuwa nzuri; hivyo akaamua kujiondoa nayo.


Vifungo/Mabano/Paradesi ( ):

a) Kuonyesha Maelezo ya Vitendo vya Msemaji/maleezo ya jukwaa
Fatuma: (Akicheka.) Umeshiba kweli!

b) Kutoa Maelezo Zaidi
Amin(alituzwa na rais) amepandishwa cheo.


Herufi Kubwa (H):

Mwanzoni mwa Sentensi
“Twendeni zetu,” akatwambia.

Baada ya alama hisi katika sentensi hisishi.

  • Salale! Umepoteza pesa zote.

Mwanzoni mwa Nomino za Pekee
Hadija, Kenya, Uganda, Jumamosi

Ufupisho wa Maneno
C.C.M (Chama cha Mapinduzi)


Koloni/Nukta Mbili (:)

a) Kuonyesha Orodha
Ili kuandaa samosa, unahitaji viungo vifuatavyo: unga, nyama, chumvi, mafuta, na kitunguu.

b) Kuandika Mazungumzo
Rhoda: Umekawia wapi?

c) Kutenganisha Saa na Dakika
7:45


Hisi/Mshangao (!):

Kuamrisha
Kachezeeni nje!

Baada ya Vihisishi
Masalaale! Pesa zangu zote zimeibwa.


Kiulizo (?):

Mwisho wa Sentensi ya ulizi
Umetoka wapi?


Herufi Nzito (h):

Kusisitiza
Jibu maswali manne pekee.


Herufi za Mlazo/Italiki (h):

Kuonyesha Neno la Kigeni
Tumealikwa na President.


Kinyota (*):

Kuonyesha neno fulani limeendelezwa Vibaya

Nipe shilingi *isirini.