Tag Archives: yambwa

Aina za shamirisho

SHAMIRISHO

Shamirisho ni nomino ambayo huashiria kitendwa/mtendwa au kitendewa/mtendewa katika sentensi.

Nomino hii huweza kuambatana na kivumishi/vivimushi.


Aina za shamirisho

Kuna aina tatu za shamirisho

  1. Shamirisho kipozi/yambwa tendwa
  2. Shamirisho kitondo/yambwa tendewa/yambiwa
  3. Shamirisho ala

Shamirisho kipozi (direct object)

Ni nomino ambayo hupokea athari ya kitenzi moja kwa moja

Mifano;

  1. Mama anapika chakula.
  2. Mama anapika chakula kitamu
  3. Mama anapika chakula kitamu sana

Chakula/chakula kitamu/chakula kitamu sana ni shamirisho kipozi kwa sababu chakula kinatendwa/kinapokea kitendo moja kwa moja.

Mifano zaidi

  1. Nyumba kubwa iliyojengwa jana imebomoka.
  2. Anita alimkatia mtoto mkate kwa kisu.
  3. Mwanaheri alinunua simu yenye rangi nyingi.

Shamirisho kitondo (indirect object)

Ni nomino ambayo huathiriwa na kitendo kwa njia isiyo ya moja kwa moja.

Sentensi nyingi huwa na vitenzi katika kauli ya kutendea/kutendewa.

Mfano

  1. Anita alimkatia mtoto mkate kwa kisu.( Nani alitendewa ? mtoto)
  2. Shangazi alimnunulia babu yangu koti. (Nani alitendewa? Babu yangu)

Shamirisho ala/kitumizi

Hii ni nomino ya kifaa ambacho hutumiwa kutendea kitendo fulani

Mara nyingi  hujitokeza katika vielezi vya namna ala

Kihusishi “kwa” si sehemu ya shamirisho ala

Mfano

  1. Anita alimkatia mtoto mkate kwa kisu .(Alitumia nini kukata mkate? Kisu)
  2. Nyumba hiyo ilijengwa kwa mawe. (nyumba ilijengwa kwa kutumia nin? Mawe)
  3. Abiria watasafiri kwa basi kubwa. ( abiria watatumia nini? Basi kubwa)

Maswali

Bainisha shamirisho katika sentensi zifuatazo

  1. Alisema atamjengea mshindi nyumba ya mbao.
  2. Mgonjwa alitibiwa na daktari kwa dawa ghali.

Share this;

Dhana ya mofimu

Mofimu

Karibuni katika kipindi cha leo ili tujifunze aina, mifano na matumizi ya mofimu katika lugha ya Kiswahili.


Mofimu ni nini?

Mofimu ni kipashio kidogo katika lugha ambacho hakiwezi kugawika zaidi bila kupoteza maana yake ya kisarufi.

Tofauti ya Kiambishi na Mofimu

Ikumbukwe kuwa kiambishi ni mofimu ambayo huongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuwakilisha dhana fulani.Pia,kiambishi hujitokeza kama mofimu tegemezi. Tofauti kuu hapa ni kuwa mofimu huweza kujisimamia kiimaan(mofimu huru) ilhali kiambishi hutegemea viambishi vingine ili kukamilisha maana.

Sifa za Mofimu

Kutokana na maelezo haya tunaweza kuorodhesha sifa zifuatazo za mofimu.


1.Mofimu ni kipashio chenye maana ya kisarufi.

Ni kweli kuwa mofimu hubeba maana ya kisarufi. Vijisehemu hivi ni muhimu sana katika sarufi.

Kwa mfano, katika neno anacheka tunaweza kupata mofimu zifuatazo.

a-na-chek-w-a

Mofimu                                   Maana ya kisarufi

a                                              nafsi ya tatu umoja

na                                           wakati uliopo

chek                                         mzizi

w                                             kauli/mnyambuliko wa kitenzi

a                                              kauli tenda/kiishio


  1. Mofimu haiwezi kugawika zaidi

Mofimu tulizoziona hapo juu haziwezi kuvunjwavunjwa zaidi. Zitapoteza maana.

Ni vizuri kutofautisha silabi na mofimu.

Silabi ni kipashio cha utamkaji ilhali mofimu ni kipashio kidogo cha kisarufi chenye maana.

Kwa hivyo,tunapoonyesha mofimu katika neno tuwe makini tusionyeshe silabi.

Tazama neno lifuatalo: Anaimba

Silabi: a+na+i+mbi+wa

Silabi hutamkika,vilevile baadhi ya vijisehemu hivi havina maana ya kisarufi.

Mofimu: a-na-imb-iw-a

Sehemu hizi zina maana ya kisarufi.

Aina mbili kuu za mofimu

  1. Mofimu huru
  2. Mofimu tegemezi

Mofimu huru

Mofimu huru hujisimamia kimaana kama neno kamili.Kimsingi hili ni  neno kamili kwa sababu lina maana iliyokamilika. Haliwezi kuvunjavunjwa bila kupoteza maana yake.

Mfano: leo,simu,meza,peremende,karatasi,darasa,hukumu,jaji,picha …

TANBIHI: Maneno haya yanaweza kuambishwa na kuwa mofimu tegemezi.

Mfano: jimeza (ji+meza)


Mofimu tegemezi

Hii ni mofimu ambayo hutegemea mofimu nyingine ili kuleta maana inayokusudiwa.

Mfano ;

Mtu : m-tu,wa-tu

Komesha: kom-esh-a

Letwa : let-w-a


Majukumu ya mofimu katika neno

  1. Mzizi wa neno

Mzizi unaweza kuwa huru au funge

Mzizi huru: sahau,dharau,safiri

Mzizi funge: fung,pik,som,chek,l,ny,ch


  1. Nafsi
NAFSI UMOJA WINGI vitenzi
Ya kwanza NI TU ni-na-ok-a, tu-na-ok-a
Ya pili U M u-na-ok-a, m-na-ok-a
Ya tatu A WA a-na-ok-a, wa-na-ok-a

  1. Ngeli

a-na-li-a : a-ngeli ya A-WA

li-me-fik-a: li-ngali ya LI-YA


  1. Umoja na wingi

m-tu: m-umoja

wa-tu: wa-wingi

ma-toto: ma-wingi


  1. Hali

Me-hali timilifu-amechoka

Hu- hali ya mazoea-hucheza

a-Hali isiyodhihirika-akamatwa

po- hali ya mazoea/wakati wowote- asomapo

ki-hali ya masharti- akija


  1. Yambwa (mtendwa/shamirisho kipozi, mtendewa/yambiwa/shamirisho kitondo)

Ku- nitakuonyesha

m-nitampigia

wa-nitawakomesha


  1. Mahali

Po- aliposimama (matumizi ya po mara nyingi hujitokeza kimuktadha)

Ni –kanisani,dukani,bungeni

Ko-alikoingia

Mo-alimoingia


  1. Kiulizi

Wasemaje?

  1. Amri

Ni- someni,simameni,tokeni


  1. Kauli/mnyambuliko

Mofimu za kauli za vitenzi ni nyingi sana katika lugha ya Kiswahili.

Kwa mfano:

a-Kauli tenda: fik-a

w-kauli tendwa: som-w-a

liw-kauli tendewa: kagu-liw-a

ek-kauli tendeka: pik-ik-a

esh-kauli tendesha: wez-esh-a


  1. Vikanushi

Ku-kikanushi cha wa wakati uliopita : hakusoma

Ja-kikanushi cha hali timilifu: hajakuona

Si-kikanushi cha nafsi ya kwanza: siendi

Hu-kikanushi cha nafsi ya pili: huendi

Ha-kikanushi cha nafsi ya tatu: haendi

Namna ya kutambua mofimu za  kukanusha

Andika neno katika hali yakinifu kisha ulikanushe

Anasoma- hasomi

Amesoma-hajasoma

 Alisoma-hakusoma


  1. Kijalizo

Ku-alikuja


  1. Kiishio/kauli tenda

A:chek-a


  1. Ukubwa na udogo wa nomino

Ki-udogo: kitoto

Ji-ukubwa:jitoto


Maswali

  1. Eleza maana ya mofimu. (alama 1)
  2. Tofautisha mofimu na kiambishi. (alama 1)
  3. Tofautisha mofimu huru na mofimu tegemezi. (alama 2)
  4. Toa mifano miwili ya mofimu huru. (alama 1)
  5. Bainisha mofimu katika neno lifuatalo; (alama 3) Hatujajibiwa
Share this;