Tag Archives: viambishi

Matumizi ya viambishi na maneno maalumu


Viambishi Maalumu

Viambishi maalumu huwa na matumizi ya kipekee katika neno au sentensi. Hapa chini tutachambua aina za viambishi maalumu na mifano yake.


1. Kiambishi ‘ni’

  • a) Nafsi ya kwanza umoja
    Nitafika kesho
  • b) Mahali
    Ameenda nyumabni.
  • c) Kitenzi kishirikishi kipungufu
    Yeye ni daktari.
  • d) Wingi
    Tokeni nje.

2. Kiambishi ‘ndi’

  • Kitenzi kishirikishi kipungufu
    Yeye ndiye aliniibia pesa.

3. Kiambishi ‘ji’

  • a) Udogo
    Kitoto kinalia.
  • b) Ukubwa
    Jibwa limebweka.
  • c) Kirejeshi cha mtenda
    Alijikata makono.
  • d) Nafsi ya pili
    Jinunulie upendacho.
  • e) Kiambishi tamati cha kuundia nomino
    Mwimbaji alituzwa na mgeni wa heshima.

4. Kiambishi ‘Ki’

  • a) Kitendo ki katika hali ya kuendelea
    Tulikuwa tukila alipoingia.
  • b) Masharti/Kitendo kinategemea kingine
    Utapita mtihani ukijitahidi.
  • c) Udogo wa nomino
    Kitoto kinalia.
  • d) Ngeli
    Kiti kimevunjika.
  • e) Kitenzi kishirikishi kipungufu
    Chakula ki mezani.
  • f) Kielezi namna mfanano
    Yeye hutembea kijeshi.
  • g) Kitendo hakifanyiki kamwe
    Kitabu hiki hakisomeki.

5. Kiambishi ‘ku’

  • a) Kikanushi cha wakati uliopita
    Hakunialika.
  • b) Nafsi ya pili umoja
    Alikupigia simu jana.
  • c) Mahali kusikodhihirika
    Huko kungepakwa rangi.
  • d) Ngeli
    Kusoma kwake kunapendeza.

6. Kiambishi ‘ka’

  • a) Mfuatano wa matukio
    Tulikula chakula, tukanywa chai kisha tukalala.
  • b) Vichwa vya habari
    Mwizi kapigwa mawe.
  • c) Kutoa amri
    Kachezeeni nje!
  • d) Kitendo fulani ni tokeo la kingine
    Tulisoma kwa bidii tukapita mtihani.
  • e) Kutoa nasaha/kushauri
    Kamwombe Mola baraka.

7. Kiambishi ‘a’

  • a) Hali isiyodhihirika
    Rais wa Marekaniawasili nchini.
  • b) Vichwa vya habari
    Waziri azomewa na wananchi.
  • c) Kitendo kinaendelea
    Twasoma magazeti.
  • d) Nafsi ya tatu umoja
    Yeye atafaulu sana.
  • e) Ngeli ya A-WA
    Twiga anapendeza sana.
  • f) Kiishio/kauli tenda katika vitenzi
    Anacheza.

8. Kiambishi ‘nge/ngali’ (Masharti Yanayowezekana au Yasiyowezekana)

  • Mfano wa masharti yanayowezekana
    Ningekuwa na pesa, ningenunua kiatu.
  • Mfano wa masharti yasiyowezekana
    Laiti ningalijua nisingaliingia katika hilo basi.

9. Kiambishi ‘po’

  • a) Mahali
    Nionyeshe alipoketi.
  • b) Wakati maalumu
  • Anapotokea wanyama hutoroka.

10. Kiambishi ‘kwa’

  • a) Mahali
    Ameenda kwa Shangazi.
  • b) Jinsi
    Alisoma kwa bidii.
  • c) Sehemu ya kitu
    Amepata alama moja kwa tano katika mtihani.
  • d) Pamoja na
    Mkutano ulijaa wazee kwa vijana.
  • e) Kuonyesha kitu kilitumiwa kama kifaa
    Alikata mkate kwa kisu.
  • f) Sababu
    Aliugua kwa kunywa maji machafu.
  • h) Muda / Kipindi
    Alilia kwa nusu sana.

Maneno Maalumu

Maneno maalumu ni maneno ambayo huwa na matumizi maalumu katika sentensi. Hapa chini, tutachambua maneno maalumu na matumizi yake.


1. Ila

  • a) Isipokuwa
    Watu wote ila yeye wameenda.
  • b) Kasoro
    Hakuna kizuri kisicho na ila.

2. Labda (Pengine / Shaka)

Mfano: Haonekani siku hizi, labda amepata uhamisho.


3. Ikiwa

  • a) (Kama / Shaka)
    Tutamkuta nyumbani ikiwa amepewa likizo.
  • b) Masharti
    Mgonjwa atapona ikiwa atakunywa dawa ipasavyo.

4. Walakini

  • a) Dosari
    Gari limekamatwa kwa sababu lilikuwa na walakini.
  • b) Lakini / Bali
    Amelipa bali hajauziwa.

5. Ingawa / Ingawaje (Hata Kama)

Mfano: Nilienda kazini ingawa sikuwa na nauli.


6. Ijapokuwa / Ijapo / Japo (Hata Kama)

Mfano: Usicheze na nyoka ijapokuwa ni mdogo.


7. Jinsi


a) aina/namna/sampuli
Siwezi kula chakula jinsi hii.
b) kulingana na/kama
Alinilipa jinsi ulivyomwambia


8. Na

  • a) Kiunganishi
    Mama na baba wanalima.
  • b) Umilikaji
    Rhoda ana kitabu kizuri.
  • c) Wakati Uliopo
    Anaandika barua.
  • d) Kauli / Mnyambuliko
    Pate na Simba wanaandikiana barua.
  • e) Kuonyesha Tofauti
    Kiatu hiki ni tofauti na kile.

Hitimisho

Kwa kuelewa matumizi ya viambishi maalumu na maneno maalumu, utaweza kuboresha ufanisi wa matumizi ya lugha ya Kiswahili chako. Endelea kujifunza na kutumia mifano hii ili kuboresha ufanisi wa mawasiliano yako katika Kiswahili!


Share this;

Viambishi

Maana ya kiambishi

  • Ni mofimuinayoongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuleta maana iliyokusudiwa.
  • Kiambishi ni kipande cha neno chenye maana ya kisarufi ambacho huongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuleta maana iliyokusudiwa.

    Kuna aina mbili za viambishi

    1. Kiambishi awali
    2. Kiambishi tamati

    Kumbuka kuwa:

    Mzizi ni sehemu ya neno ambayo huongezwa viambishi.

    Mfano:

    • Wa-tu / m-toto :(nomino)
    • A-na-chez-a/ a-ta-pik-a :(kitenzi)

    Viambishi awali hutumika kuonyesha:

    1. Ngeli
    2. Kiima/mtenda
    3. Nafsi
    4. Wakati
    5. Yambwa(mtendwa/ mtendewa)
    6. Hali (timilifu/mazoea/isiyod hihirika/masharti)
    7. Kirejeshi
    8. Kikanushi
    9. Umoja/wingi
    10. Ukubwa/udogo wa nomino

    Mifano ya Vikanushi

    Viambishi tamati hutumika kuonyesha:

    1. kirejeshi
    2. kiulizi
    3. Kauli/mnyambuliko
    4. Kiishio
    5. Uundaji wa nomino

    Kubainisha viambishi

    Mfano 1

    Mfano 2

    Mfano 3

    Mfano 4

    Mfano 5

    a)Onyesha viambishi awali na viambishi tamati

    b) Bainisha majukumu ya viambishi ulivyotambua

    • ViatuWalipochezaTegewaHakumpigaAnyweshavyoAlimdharau

    • jigari

    Majibu

    1. Viatu: awali; vi
    2. Walipocheza- awali:wa,li,po tamati: a
    3. Tegewa: –                                      tamati: ew, a
    4. Hakumpiga- awali:ha,ku,m                                      tamati: a
    5. Anyweshavyo- awali: a                              tamati:esh, a, vyo
    6. alimdharau- awali:a,li,m
    7. jigari: awali; ji


    Share this;

    Dhana ya mofimu

    Mofimu

    Karibuni katika kipindi cha leo ili tujifunze aina, mifano na matumizi ya mofimu katika lugha ya Kiswahili.


    Mofimu ni nini?

    Mofimu ni kipashio kidogo katika lugha ambacho hakiwezi kugawika zaidi bila kupoteza maana yake ya kisarufi.

    Tofauti ya Kiambishi na Mofimu

    Ikumbukwe kuwa kiambishi ni mofimu ambayo huongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuwakilisha dhana fulani.Pia,kiambishi hujitokeza kama mofimu tegemezi. Tofauti kuu hapa ni kuwa mofimu huweza kujisimamia kiimaan(mofimu huru) ilhali kiambishi hutegemea viambishi vingine ili kukamilisha maana.

    Sifa za Mofimu

    Kutokana na maelezo haya tunaweza kuorodhesha sifa zifuatazo za mofimu.


    1.Mofimu ni kipashio chenye maana ya kisarufi.

    Ni kweli kuwa mofimu hubeba maana ya kisarufi. Vijisehemu hivi ni muhimu sana katika sarufi.

    Kwa mfano, katika neno anacheka tunaweza kupata mofimu zifuatazo.

    a-na-chek-w-a

    Mofimu                                   Maana ya kisarufi

    a                                              nafsi ya tatu umoja

    na                                           wakati uliopo

    chek                                         mzizi

    w                                             kauli/mnyambuliko wa kitenzi

    a                                              kauli tenda/kiishio


    1. Mofimu haiwezi kugawika zaidi

    Mofimu tulizoziona hapo juu haziwezi kuvunjwavunjwa zaidi. Zitapoteza maana.

    Ni vizuri kutofautisha silabi na mofimu.

    Silabi ni kipashio cha utamkaji ilhali mofimu ni kipashio kidogo cha kisarufi chenye maana.

    Kwa hivyo,tunapoonyesha mofimu katika neno tuwe makini tusionyeshe silabi.

    Tazama neno lifuatalo: Anaimba

    Silabi: a+na+i+mbi+wa

    Silabi hutamkika,vilevile baadhi ya vijisehemu hivi havina maana ya kisarufi.

    Mofimu: a-na-imb-iw-a

    Sehemu hizi zina maana ya kisarufi.

    Aina mbili kuu za mofimu

    1. Mofimu huru
    2. Mofimu tegemezi

    Mofimu huru

    Mofimu huru hujisimamia kimaana kama neno kamili.Kimsingi hili ni  neno kamili kwa sababu lina maana iliyokamilika. Haliwezi kuvunjavunjwa bila kupoteza maana yake.

    Mfano: leo,simu,meza,peremende,karatasi,darasa,hukumu,jaji,picha …

    TANBIHI: Maneno haya yanaweza kuambishwa na kuwa mofimu tegemezi.

    Mfano: jimeza (ji+meza)


    Mofimu tegemezi

    Hii ni mofimu ambayo hutegemea mofimu nyingine ili kuleta maana inayokusudiwa.

    Mfano ;

    Mtu : m-tu,wa-tu

    Komesha: kom-esh-a

    Letwa : let-w-a


    Majukumu ya mofimu katika neno

    1. Mzizi wa neno

    Mzizi unaweza kuwa huru au funge

    Mzizi huru: sahau,dharau,safiri

    Mzizi funge: fung,pik,som,chek,l,ny,ch


    1. Nafsi
    NAFSI UMOJA WINGI vitenzi
    Ya kwanza NI TU ni-na-ok-a, tu-na-ok-a
    Ya pili U M u-na-ok-a, m-na-ok-a
    Ya tatu A WA a-na-ok-a, wa-na-ok-a

    1. Ngeli

    a-na-li-a : a-ngeli ya A-WA

    li-me-fik-a: li-ngali ya LI-YA


    1. Umoja na wingi

    m-tu: m-umoja

    wa-tu: wa-wingi

    ma-toto: ma-wingi


    1. Hali

    Me-hali timilifu-amechoka

    Hu- hali ya mazoea-hucheza

    a-Hali isiyodhihirika-akamatwa

    po- hali ya mazoea/wakati wowote- asomapo

    ki-hali ya masharti- akija


    1. Yambwa (mtendwa/shamirisho kipozi, mtendewa/yambiwa/shamirisho kitondo)

    Ku- nitakuonyesha

    m-nitampigia

    wa-nitawakomesha


    1. Mahali

    Po- aliposimama (matumizi ya po mara nyingi hujitokeza kimuktadha)

    Ni –kanisani,dukani,bungeni

    Ko-alikoingia

    Mo-alimoingia


    1. Kiulizi

    Wasemaje?

    1. Amri

    Ni- someni,simameni,tokeni


    1. Kauli/mnyambuliko

    Mofimu za kauli za vitenzi ni nyingi sana katika lugha ya Kiswahili.

    Kwa mfano:

    a-Kauli tenda: fik-a

    w-kauli tendwa: som-w-a

    liw-kauli tendewa: kagu-liw-a

    ek-kauli tendeka: pik-ik-a

    esh-kauli tendesha: wez-esh-a


    1. Vikanushi

    Ku-kikanushi cha wa wakati uliopita : hakusoma

    Ja-kikanushi cha hali timilifu: hajakuona

    Si-kikanushi cha nafsi ya kwanza: siendi

    Hu-kikanushi cha nafsi ya pili: huendi

    Ha-kikanushi cha nafsi ya tatu: haendi

    Namna ya kutambua mofimu za  kukanusha

    Andika neno katika hali yakinifu kisha ulikanushe

    Anasoma- hasomi

    Amesoma-hajasoma

     Alisoma-hakusoma


    1. Kijalizo

    Ku-alikuja


    1. Kiishio/kauli tenda

    A:chek-a


    1. Ukubwa na udogo wa nomino

    Ki-udogo: kitoto

    Ji-ukubwa:jitoto


    Maswali

    1. Eleza maana ya mofimu. (alama 1)
    2. Tofautisha mofimu na kiambishi. (alama 1)
    3. Tofautisha mofimu huru na mofimu tegemezi. (alama 2)
    4. Toa mifano miwili ya mofimu huru. (alama 1)
    5. Bainisha mofimu katika neno lifuatalo; (alama 3) Hatujajibiwa
    Share this;