Tag Archives: mofimu

Viambishi

Maana ya kiambishi

  • Ni mofimuinayoongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuleta maana iliyokusudiwa.
  • Kiambishi ni kipande cha neno chenye maana ya kisarufi ambacho huongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuleta maana iliyokusudiwa.

    Kuna aina mbili za viambishi

    1. Kiambishi awali
    2. Kiambishi tamati

    Kumbuka kuwa:

    Mzizi ni sehemu ya neno ambayo huongezwa viambishi.

    Mfano:

    • Wa-tu / m-toto :(nomino)
    • A-na-chez-a/ a-ta-pik-a :(kitenzi)

    Viambishi awali hutumika kuonyesha:

    1. Ngeli
    2. Kiima/mtenda
    3. Nafsi
    4. Wakati
    5. Yambwa(mtendwa/ mtendewa)
    6. Hali (timilifu/mazoea/isiyod hihirika/masharti)
    7. Kirejeshi
    8. Kikanushi
    9. Umoja/wingi
    10. Ukubwa/udogo wa nomino

    Mifano ya Vikanushi

    Viambishi tamati hutumika kuonyesha:

    1. kirejeshi
    2. kiulizi
    3. Kauli/mnyambuliko
    4. Kiishio
    5. Uundaji wa nomino

    Kubainisha viambishi

    Mfano 1

    Mfano 2

    Mfano 3

    Mfano 4

    Mfano 5

    a)Onyesha viambishi awali na viambishi tamati

    b) Bainisha majukumu ya viambishi ulivyotambua

    • ViatuWalipochezaTegewaHakumpigaAnyweshavyoAlimdharau

    • jigari

    Majibu

    1. Viatu: awali; vi
    2. Walipocheza- awali:wa,li,po tamati: a
    3. Tegewa: –                                      tamati: ew, a
    4. Hakumpiga- awali:ha,ku,m                                      tamati: a
    5. Anyweshavyo- awali: a                              tamati:esh, a, vyo
    6. alimdharau- awali:a,li,m
    7. jigari: awali; ji


    Share this;

    Dhana ya mofimu

    Mofimu

    Karibuni katika kipindi cha leo ili tujifunze aina, mifano na matumizi ya mofimu katika lugha ya Kiswahili.


    Mofimu ni nini?

    Mofimu ni kipashio kidogo katika lugha ambacho hakiwezi kugawika zaidi bila kupoteza maana yake ya kisarufi.

    Tofauti ya Kiambishi na Mofimu

    Ikumbukwe kuwa kiambishi ni mofimu ambayo huongezwa kabla au baada ya mzizi wa neno ili kuwakilisha dhana fulani.Pia,kiambishi hujitokeza kama mofimu tegemezi. Tofauti kuu hapa ni kuwa mofimu huweza kujisimamia kiimaan(mofimu huru) ilhali kiambishi hutegemea viambishi vingine ili kukamilisha maana.

    Sifa za Mofimu

    Kutokana na maelezo haya tunaweza kuorodhesha sifa zifuatazo za mofimu.


    1.Mofimu ni kipashio chenye maana ya kisarufi.

    Ni kweli kuwa mofimu hubeba maana ya kisarufi. Vijisehemu hivi ni muhimu sana katika sarufi.

    Kwa mfano, katika neno anacheka tunaweza kupata mofimu zifuatazo.

    a-na-chek-w-a

    Mofimu                                   Maana ya kisarufi

    a                                              nafsi ya tatu umoja

    na                                           wakati uliopo

    chek                                         mzizi

    w                                             kauli/mnyambuliko wa kitenzi

    a                                              kauli tenda/kiishio


    1. Mofimu haiwezi kugawika zaidi

    Mofimu tulizoziona hapo juu haziwezi kuvunjwavunjwa zaidi. Zitapoteza maana.

    Ni vizuri kutofautisha silabi na mofimu.

    Silabi ni kipashio cha utamkaji ilhali mofimu ni kipashio kidogo cha kisarufi chenye maana.

    Kwa hivyo,tunapoonyesha mofimu katika neno tuwe makini tusionyeshe silabi.

    Tazama neno lifuatalo: Anaimba

    Silabi: a+na+i+mbi+wa

    Silabi hutamkika,vilevile baadhi ya vijisehemu hivi havina maana ya kisarufi.

    Mofimu: a-na-imb-iw-a

    Sehemu hizi zina maana ya kisarufi.

    Aina mbili kuu za mofimu

    1. Mofimu huru
    2. Mofimu tegemezi

    Mofimu huru

    Mofimu huru hujisimamia kimaana kama neno kamili.Kimsingi hili ni  neno kamili kwa sababu lina maana iliyokamilika. Haliwezi kuvunjavunjwa bila kupoteza maana yake.

    Mfano: leo,simu,meza,peremende,karatasi,darasa,hukumu,jaji,picha …

    TANBIHI: Maneno haya yanaweza kuambishwa na kuwa mofimu tegemezi.

    Mfano: jimeza (ji+meza)


    Mofimu tegemezi

    Hii ni mofimu ambayo hutegemea mofimu nyingine ili kuleta maana inayokusudiwa.

    Mfano ;

    Mtu : m-tu,wa-tu

    Komesha: kom-esh-a

    Letwa : let-w-a


    Majukumu ya mofimu katika neno

    1. Mzizi wa neno

    Mzizi unaweza kuwa huru au funge

    Mzizi huru: sahau,dharau,safiri

    Mzizi funge: fung,pik,som,chek,l,ny,ch


    1. Nafsi
    NAFSI UMOJA WINGI vitenzi
    Ya kwanza NI TU ni-na-ok-a, tu-na-ok-a
    Ya pili U M u-na-ok-a, m-na-ok-a
    Ya tatu A WA a-na-ok-a, wa-na-ok-a

    1. Ngeli

    a-na-li-a : a-ngeli ya A-WA

    li-me-fik-a: li-ngali ya LI-YA


    1. Umoja na wingi

    m-tu: m-umoja

    wa-tu: wa-wingi

    ma-toto: ma-wingi


    1. Hali

    Me-hali timilifu-amechoka

    Hu- hali ya mazoea-hucheza

    a-Hali isiyodhihirika-akamatwa

    po- hali ya mazoea/wakati wowote- asomapo

    ki-hali ya masharti- akija


    1. Yambwa (mtendwa/shamirisho kipozi, mtendewa/yambiwa/shamirisho kitondo)

    Ku- nitakuonyesha

    m-nitampigia

    wa-nitawakomesha


    1. Mahali

    Po- aliposimama (matumizi ya po mara nyingi hujitokeza kimuktadha)

    Ni –kanisani,dukani,bungeni

    Ko-alikoingia

    Mo-alimoingia


    1. Kiulizi

    Wasemaje?

    1. Amri

    Ni- someni,simameni,tokeni


    1. Kauli/mnyambuliko

    Mofimu za kauli za vitenzi ni nyingi sana katika lugha ya Kiswahili.

    Kwa mfano:

    a-Kauli tenda: fik-a

    w-kauli tendwa: som-w-a

    liw-kauli tendewa: kagu-liw-a

    ek-kauli tendeka: pik-ik-a

    esh-kauli tendesha: wez-esh-a


    1. Vikanushi

    Ku-kikanushi cha wa wakati uliopita : hakusoma

    Ja-kikanushi cha hali timilifu: hajakuona

    Si-kikanushi cha nafsi ya kwanza: siendi

    Hu-kikanushi cha nafsi ya pili: huendi

    Ha-kikanushi cha nafsi ya tatu: haendi

    Namna ya kutambua mofimu za  kukanusha

    Andika neno katika hali yakinifu kisha ulikanushe

    Anasoma- hasomi

    Amesoma-hajasoma

     Alisoma-hakusoma


    1. Kijalizo

    Ku-alikuja


    1. Kiishio/kauli tenda

    A:chek-a


    1. Ukubwa na udogo wa nomino

    Ki-udogo: kitoto

    Ji-ukubwa:jitoto


    Maswali

    1. Eleza maana ya mofimu. (alama 1)
    2. Tofautisha mofimu na kiambishi. (alama 1)
    3. Tofautisha mofimu huru na mofimu tegemezi. (alama 2)
    4. Toa mifano miwili ya mofimu huru. (alama 1)
    5. Bainisha mofimu katika neno lifuatalo; (alama 3) Hatujajibiwa
    Share this;

    Maana ya mzizi wa neno

    Dhana ya mzizi wa neno

    mfano wa mzizi

    Tunaposikia neno mzizi jambo la kwanza ambalo hutujia akilini ni sehemu fulani ya mti.Mti  husimama na kukua kwa sababu umeshikiliwa ardhini na mizizi.Hivyo basi,neno huitaji mzizi.

    Sehemu hii ni muhimu sana katika neno kwani hubeba maana ya kimsingi ya neno fulani.Kwa mfano kutokana na mzizi –tu tunaweza kupata maneno kama; mtu,watu,kitu,vitu. Kwa hivyo, mzizi hutumiwa tunapounda maneno katika lugha.Sehemu hii pia haibadiliki hata neno likiongezwa viambishi.

    Kwa mfano:

    • Wanaochekwa,tuliowacheka (mzizi ni chek)
    • Vilivyosomwa,someana,somesha,somwa

    Kutokana na mifano hii tunaweza kusema mzizi ni sehemu ya neno ambayo huongezwa viambishi au sehemu ambayo hubakia baada ya kuondoa viambishi awali na tamati.

    Kutambua mzizi katika neno

    Jambo la kwanza ni kuondoa viambishi.

    Kwa mfano: waliangukia

    Wa-li-anguk-i-a ,mzizi ni anguk

    Aina za mzizi

    Katika lugha ya Kiswahili kuna mzizi huru na mzizi funge.Mzizi huru huwa neno kamili bila kuongezwa viambishi.Kwa mfano,leo,kamusi,sahau,dharau.. Mzizi funge huongezwa viambishi ili kuwa na maana kamili,kwa mfano anguk,som,on,pig,andik,f,l,ch, …

    Maswali

    Onyesha mzizi katika maneno yafuatayo

    1. nywishiana
    2. Alinijia
    3. Pakuliwa
    4. Oneana
    5. Safirishiwa
    6. Valiana
    7. pokezwa
    Share this;