Kueleza maana ya silabi na kutunga maneno
Tag Archives: irabu
Uainishaji wa irabu
Mwandishi: Zablon Rogito
SAUTI
Maana: Sauti ni mlio unaotokana na mgusano wa ala za kutamkia wakati wa kuzungumza
Aina za sauti
Sauti za lugha ya kiswahili zimegawika katika makundi mawili:
- Irabu
- Konsonanti
Irabu
Irabu ni sauti ambazo inapotamkwa hewa kutoka mapafuni haizuiliwi Kwokwote, yaani hewa upita kwa ulaini.
Sauti za irabu ni tano nazo ni:
/a/,/e/,/i/,/o/,/u/
Vigezo vya kuainisha irabu
Irabu uainishwa kwa kuzingatia Vigezo vifutavyo
1. Hali ya midomo
- Mviringo: u,a
- Kutandazika: a,i,e
2. Mkao wa ulimi katika kinywa
- Juu: u,i
- Chini: a
- Kati: o,e
3. Sehemu ya ulimi ya kutamkia
- Mbele: e,i
- Kati: a
- Nyuma: u,o
Sauti na sifa zake bainifu
/a/_hutamkiwa chini kati
_inapotamkwa midomo utandazika
/e/_hutamkiwa mbele kati
_midomo utandazika
/i/_hutamkiwa mbele juu
_midomo utandazika
/o/_hutamkiwa nyuma kati
_midomo huwa mviringo
/u/_ni sauti ya nyuma juu
_inapotamkwa midomo huviringika
Aina na miundo ya silabi
Silabi ni kipashio kinachotamkika
Maana
Sauti mbili au zaidi zinazotamkwa kwa pamoja.
Sauti mbili au zaidi ambazo hutamkwa kama fungu moja la sauti.
Aina za silabi
Kuna aina mbili za sila katika Kiswahili
Silabi funge
Hizi ni silabi ambazo huishwa kwa konsonanti
Mfano: m-tu
Silabi wazi/huru
Hizi ni silabi ambazo huishia kwa irabu
Mfano: ka-ka, le-o,u-si-ku
MUUNDO WA SILABI
Kuna miundo mbalimbali ya silabi katika Kiswahil
Irabu pekee
o-a,i-ta
konsonanti pekee
m-tu
konsonanti irabu
ji-tu
konsonanti konsonanti irabu
fye-ka, bwe-ka
konsonanti konsonanti konsonanti irabu
mbwe-ha,twa-ngwa
Mifano ya maswali
- Eleza maana ya silabi.(alama 1)
- Huku ukitoa mifano eleza aina mbili za silabi. (alama 2)
- Eleza miundo yoyote miwili ya silabi. (alama 2)
- Tenganisha silabi: viyeyusho (alama 2)
- Tunga neno lenye muundo ufuatao: KI+KI+I. (alama 2)
