Tag Archives: chopi

Maswali na majibu: Kigogo

Jamii imemkandamiza mwanamke.

Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea Tamthilia ya Kigogo.

1. Kudharauliwa

Majoka anasema wanawake ni wanawake tu.

2. Kutumiwa kama chombo cha mapenzi

Majoka anataka kuishiriki mapenzi na Ashua kama kigezo cha kumpa msaada.

3. Kupigwa

Tunu anapigwa na kuvunjwa mguu na Chopi,Ngurumo na vijana wengine.

4. Kutusiwa

Majoka anasema « sina time ya wanawake »

5. Kufungwa bila hatia

Majoka anamfunga Ashua kwa madai ya kuzua vurugu katika ofisi ya serikali.Ilikuwa ni njia ya kulipiza kisasi kwa Sudi na kumnasa Ashua.

6. Kunyimwa kura

Tunu anapoenda mangweni kujaribu kuwakomboa walevi wamuimbia nyimbo za kumkejeli. Ngurumu anadai kuwa hawezi kumpa mwanamke kura.

7. Kutopewa nafasi ya uongozi katika jamii

Kenga anamwuliza Sudi iwapo Sagamayo ishawahi kuwa na Shujaa wa kike.

8. Kupangiwa njama ya kuuwawa

Kenga na Majoka wanapanga njama ya kumwangamiza Tunu.Wanawatuma vijana,akiwepo Chopi kumwangamiza lakini wanamvunja mguu.

9. Kuishi kwa hofu

Hashima anasema kuwa yeye na Tunu wake wanaishi kwa hofu,kila waamkapo wanapiga alhamdulillahi.

10. Kusalitiwa katika ndoa

Majoka anasema kuwa hampendi Husda bali alimwoa ili kutimiza wajibu wake kama kiongozi.Majoka anampenda Ashua.

Maswali mengine


Share this;

Majibu: Swali la Dondoo

MAJIBU
“Sina muda wa kufikiria mambo ya watu…nafikiria maneno matamu kama asali”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)

i. Maneno ya Majoka
ii. Msemewa ni Chopi
iii. Mahali ni Majoka and Majoka Modern Resort
iv. Majoka amefahamishwa kifo cha Ngurumo na Chopi ni kusema afukiwe juu ya wengine.
v. Majoka ametoa amri kuwa chatu mmoja atolewe kafara ili wakereketwa wa mazingira waanze kuandamana hivyo basi kamera hazitaelekezwa makaburini

b) Fafanua sifa zozote sita za msemewa katika kauli hii. (alama 6)

i. Mtiifu/mwaminifu – anamheshimu Majoka na kufuata amri zake kikamilifu.Alifuata amri ya kumkamata Ashua.
ii. Mkatili– alishiriki katika kumvunja Tunu mguu. Alikuwa amepewa amri ya kumwangamiza.
iii. Ni mpyoro– anamwita Sudi ngiri
iv. Ni kikaragosi– anatumiwa na Majoka kuendeleza utawala wa kidhalimu. Anahusika katika kumvamia Tunu na kumvunja mguu kwani Tunu anapinga uongozi wa Majoka.
v. Ni mwenye kiburi– anamkemea Sudi na kumwambia atoke katika chumba cha wafungwa na iwapo ameshindwa kumtunza Ashua amwambie.
vi. Ni mslati – walinzi wa Majoka wanapomwona Kingi akibebwa na kushangilia na umati wanaacha kumlinda Majoka.Chopi ni mlinzi wa Majoka.

c) Onyesha kinyume kinachojitokeza katika kauli hii. (alama 2)
Majoka anasema hana muda wa kumfikiria Ngurumo ilhali alikuwa mfuasi wake

d) Fafanua matumizi mengine ya mbinu hii katika tamthilia (alama 8)

i. Ni kinaya kuwa serikali ya Majoka inakusanya kodi lakini soko ni chafu.
ii. Sudi anasema kuwa serikali ya majoka inachukua kilicho chao na kuwatisha.
iii. Katinga matangazo ya redio wanasagamoyo wanatangaziwa kipindi cha mwezi mmoja cha kusherehekea ufanisi wao- hakuna ufanisi Sagamoyo,soko ni chafu,kuna maandamano na watawaliwa kutishwa.
iv. Ngurumo ni mfuasi sugu wa Majoka lakini anapokufa Majoka anasema afukiwe juu ya wengine na hana muda wa kufikiria mambo ya watu.
v. Chopi ni mwaminifu kwa Majoka lakini aliposhindwa kumwangamiza Tunu Kenga na Majoka wana njama ya kumwangamiza.
vi. Ngurumo anasema kuwa pombe inawapa starehe lakini kuna watu wamekuwa vipofu.
vii. Kenga anamwambia Majoka aache moyo wa huruma ingawaje Majoka anatoa amri ya kunyanyasa raia.Anasema atamkomesha Tunu.Pia,anamwambia Kingi awapige wananchi risasi.
viii. Boza anasema kulipa kodi ni kujenga nchi na kujitegemea ilhali mradi wa kuchonga kinyago umefadhiliwa kutoka nje.Pia wananchi hawana chakula,Ashua anaenda kwa Majoka kuomba chakula.

Share this;