Maswali ya insha

Andika insha MBILI. Insha ya KWANZA ni ya LAZIMA.

Chagua insha moja nyingine kutoka tatu zilizobaki.

Kila Insha isipungue maneno 400.

Kila Insha ina alama 20.

Maswali

  1. Lazima

Umepewa ratiba ya tamasha za muziki baina ya shule za upili katika eneo lako.Andika shajara ya matukio ya juma moja.

2. Mfumo wa ugatuzi nchini Kenya una faida nyingi kuliko hasara.Jadili.

3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo:

                Mpiga ngumi ukuta ,huumiza mkonowe.

4. Tunga kisa kinachomalizika kwa maneno yafuatayo:

…kwa kweli nilikuwa nimeanguka kitakotako,nilijuta sana!

MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA

  1. Lazima

Umepewa ratiba ya tamasha za muziki baina ya shule za upili katika eneo lako.Andika shajara ya matukio ya juma moja.

  1. SURA
  2. Anwani- iwe na maneno: SHAJARA YA TAMASHA ZA MUZIKI KATIKA …
  3. Anwani iandikwe kwa herufi kubwa.
  4. Mahali pa kuandalia tamasha hizi patajwe.
  5. Muda utakaochukuliwa uonyeshwe(juma zima) japo si lazima hapa.
  6. Siku,tarehe,mwezi na mwaka uandikwe kama vijimada vidogovidogo vya siku zote saba za juma moja.
  7. Matukio mbalimbali yanayotazamiwa kutekelezwa yaonyeshwe.
  • MAUDHUI

Mtahiniwa aonyeshe vitengo mbalimbali vya matukio yatakayoshughulikiwa kila siku.

Mambo haya yahusishwe:

  1. Kwaya- nyimbo za dini,muziki wa ala/taarab
  2. Densi za kitamaduni
  3. Mashairi- Kiingereza,Kiswahili,Kifaransa na lugha nyinginezo. K.m shairi la mtu mmoja,watu wawili.n.k.

Anaweza  kutaja aina zozote za ushairi k.v,maghani,malumbano na ngonjera.

  1. Mazungumzo ya ghafla.
  2. Kusoma makala
  3. Michezo ya kuigiza ya kimuziki

*katika vitengo vilivyotajwa mtahiniwa anaweza kugusia maswala ibuka k.v,

  1. Dawa za kulevya
  2. Urithi wa wajane
  3. Ugaidi
  4. Ukeketaji
  5. Uchaguzi
  6. Ufisadi
  7. Siasa
  8. Ubaguzi wa kijinsia/ubabedume
  9. Ajira ya watoto
  10. Dini

KIELELEZO

SHAJARA YA TAMASHA ZA MUZIKI ZITAKAZOANDALIWA KATIKA SHULE YA UPILI  YA LENGA JUU KUANZIA TAREHE 20-27 JUNI 2016.

Jumatatu 20/06/16

Pataandaliwa mashindano ya miziki ya injili,taarab,ala na kitamaduni katika madaraja mbalimbali.Shule kadhaa za wasichana na wavulana zitashiriki.

Jumanne  21/06/16

Densi za kitamaduni katika jamii mbalimbali zitaandaliwa.Densi za Afrika Mashariki zitaandaliwa majira ya asubuhi na za Afrika Magharibi zitaandaliwa mwendo wa alasiri.

Jumatano  22/06/16

Mashairi ya aina mbalimbali yataghanwa na kukaririwa.Mashairi ya Kiingereza yatashughulikiwa majira ya asubuhi,ya Kiswahili na lugha nyinginezo za Kiafrika majira ya alasiri na ya Kifaransa jioni.

Alhamisi  23/06/16                    

Washiriki watapewa mada fulani fulani za maswala ibuka ili wazijadili chini ya kitengo cha mazungumzo ya ghafla kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne.

Ijumaa 24/06/16

Washiriki watapewa makala fulani kuhusu masuala ibuka ili waweze kuyasoma kwa sauti na ufasaha wa hali ya juu.

Jumamosi 25/06/16

Mashindano ya bendi za kugongana  baina ya shule za mseto za eneo hili la Bondeni.

Jumapili 26/06/16

Matangazo ya matokeo.

Kutuzwa kwa makundi yaliyoshinda.

Kufungwa kwa sherehe hii kirasmi.

TANBIHI

  • Hiki ni kielelezo tu.Mtahiniwa ana uhuru wa kupanga matukio yake kwa njia nyingine yoyote ile inayokubalika mradi asipotoke.
  • Asiandike ratiba.Akifanya hivyo atuzwe bakshishi 01.
  • Wajaze angaa pande mbili za karatasi ya majibu.
  • Mfumo wa ugatuzi nchini Kenya una faida nyingi kuliko hasara.Jadili.
  • Mtahini anastahili kujadili kuhusu faida na hasara za mfumo huu wa uongozi
  • Itakuwa bora akitanguliza kwa kueleza maana ya ugatuizi japo si lazima.
  • Baada ya kujadili pande zote mbili ,mtahiniwa  atoe msimamo wake.
  • Mtahiniwa akijadili upande mmoja tu wa swali hili asituzwe zaidi ya alama kumi (10) zilizotengewa swali.

Maana ya ugatuzi

Ni mfumo wa utawala au uongozi ambapo mamlaka huwa yemeenezwa katika majimbo au mashinani ili kuhakikisha kuwa huduma muhimu zimewafikia wananchi kote nchini.

FAIDA

  1. Unarahishisha uongozi au utawala nchini. Kwa mfano,kila jimbo limekuwa na gavana wake
  2. Unazalisha nafasi nyingi za ajira hasa mashinani  k.m, wawakilishi wa wadi n.k
  3. Unaimarisha kiwango cha uchumi katika majimbo tofauti kote nchini.
  4. Unahakikisha kila gatuzi/jimbo linajiendeleza kwa mfano ujenzi wa barabara,hospitali na miundo-msingi mingine.
  5. Unaboresha kiwango cha elimu katika majimbo yote na nchi kwa jumla.
  6. Unaimarisha usalama.
  7. Wananchi wamehusishwa katika utawala.

HASARA

  1. Mfumo huu unatumia pesa nyingi katika kugharimia mishahara  ya wananchi ambao wameajiriwa katika magatuzi mbalimbali.
  2. Umezua mgogoro kati ya utawala wa kitaifa na utawala wa majimbo.
  3. Umezua ukabila kwa kuwa Wakenya wanaamini kuwa kila mtu ni sharti aishi na aajiriwe kazi katika jimbo alimozaliwa na kulelewa.
  4. Majimbo mengine yamekosa kuendelea kutokana na uongozi mbaya.
  5. Majimbo mengine yamebakia nyuma kimaendeleo kwa sababu hayana rasilimali za kutosha.
  6. Ufisadi umekithiri.
  7. Ubadhirifu wa pesa za umma k.m,starehe nyingi k.v,ziara katika mataifa ya nje zisizo na faida yoyote.
  8. Ahadi zisizotimizika.
  • Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo:

                  Mpiga ngumi ukuta ,huumiza mkonowe.

  • Mada iwe methali hii.Akiandika anwani tofauti aondolewe alama za mtindo.
  • Si lazima atangulize kwa kueleza maana ya methali hii.Si kosa akifanya hivyo.
  • Ashughulikie pande zote mbili za methali.Asipofanya hivyo ,asituzwe zaidi ya alama 10.
  • Asimulie kisa kinacholenga maana ya methali hii.

Maana:            Ajitakiaye msiba hana kilio labda alie na mizimu wake tu.

Matumizi:       – Hutumiwa kumnasihi na kumwonya mtu asishindane na mtu anayemzidi uwezo kwa   kuwa akifanya hivyo atajiumiza bure.

  • Anayejitakia msiba kisha akaanza kuwalaumu wengine kwa kutomsikitikia ndiye huambiwa methali hii.
  • Tunga kisa kinachomalizika kwa maneno yafuatayo:

           …kwa kweli nilikuwa nimeanguka kitakotako,nilijuta sana!

  • Aandike kichwa – abuni na kisizidi maneno sita.
  • Asiongeze au adondoe neno au herufi katika mdokezo  huu.Akifanya hivyo atuzwe bakshishi 01.
  • Lazima maneno ya mdokezo yaje mwisho kabisa.
  • Mtahiniwa asimulie kisa kitakachohusisha mhusika ambaye mambo yamemharibikia au kumwendea kombo kwa sababu ya kosa lake mwenyewe.

                          Au

  • Asimulie kisa kuhusu mhusika ambaye alikuwa amenawiri kimaisha baadaye mafanikio yake kusambaratika kwa sababu ya mwelekeo potovu aliouchukuwa.

UKADIRIAJI NA UTUZAJI

                                                                                                                              Alama

  Maneno 174                                                 Insha robo          ____________04-05

  Maneno 175-274                                        Insha nusu           ____________ 10

   Maneno 275-374                                       Insha robo tatu    ____________15

    Maneno 375 na kuendelea                       Insha kamili          ____________ 20       

Maudhui07-08           A05-06       B03-04     C01-02    D
Jumla ya Upeo16-2011-1506-1001-05

Umuhimu wa maswali balagha katika fasihi

Maswali ya balagha ni maswali ambayo hayahitaji jibu moja kwa moja. Yanaweza kutumika kuchochea fikira, kusisitiza hoja, au kuonyesha hisia fulani. 

Umuhimu wa maswali balagha

Umuhimu wa Maswali Balagha katika Ushairi:

Kuchochea Fikra

  • Maswali balagha yanawafanya wasomaji au wasikilizaji kutafakari kwa kina juu ya mada inayozungumziwa. Yanaleta nafasi ya kujitafakari na kuchunguza maana nzito ndani ya ushairi.

Kuongeza Msisitizo

    • Hutumika kuimarisha ujumbe wa mshairi. Kwa kuuliza maswali ambayo hayahitaji majibu, mshairi anaweza kusisitiza hisia au maoni fulani kwa nguvu zaidi.

    Kueleza Hisia

      • Maswali balagha yanaweza kuonyesha hisia za mshairi kama mshangao, huzuni, au furaha. Hutumiwa kuonesha machungu au furaha kwa njia ambayo inagusa hisia za msomaji.

      Kuvutia Hadhira

        • Maswali balagha hujenga mvuto na kuamsha shauku ya msomaji au msikilizaji. Ni njia ya kumfanya msomaji ajihusishe zaidi na mashairi, kwani maswali yanampa nafasi ya kushiriki kiakili.

        Kufichua Uhalisia

          • Mara nyingi maswali balagha yanaibua ukweli kuhusu masuala ya kijamii, kimaadili, au kisiasa kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Hii husaidia kueleza uhalisia bila kulazimisha au kuamrisha.

            Iwapo utahitajika kuelezea majukumu ya maswali balagha katika ushairi au kitabu itakulazimu urejelee sehemu swali hilo lilipotumika ili upate matumizi yake kamili.

            Visasili

            Visasili na hadithi ambazo huelezea chanzo cha jambo au tukio fulani katika jamii. Aghalabu,huandamana na imani za kidini za kijamii.

            Mfano wa kisasili

            Hapo zamani za kale, wakati dunia ilikuwa bado changa, kulikuwa na Mungu mmoja aitwaye Mumba, ambaye ndiye aliyetengeneza kila kitu kilichoonekana na kisichoonekana. Mumba alikuwa na nguvu na hekima nyingi, na aliumba dunia, mbingu, maji, na mimea yote kwa nguvu ya neno lake tu.


            Baada ya kuumba ardhi na anga, Mumba aliamua kuumba kiumbe atakayekuwa mwakilishi wake duniani. Alikusanya udongo wenye rutuba kutoka kwenye kingo za mto mkubwa na kuupaka kwa maji matakatifu. Aliufinyanga udongo huo kwa mikono yake mwenyewe, akiunda kiumbe kilichokuwa na sura nzuri na kiwiliwili thabiti. Aliupa kiumbe huyu jina la Mtu.


            Lakini Mumba alijua kwamba udongo na maji havitoshi kumpa Mtu uzima wa kweli. Kwa hivyo, alielekea kwenye mti mtakatifu uliokuwa na mizizi yenye nguvu za maisha, na kutoka humo, alitoa pumzi ya uhai. Alipuliza pumzi hiyo kwenye pua za Mtu, na hapo Mtu akafungua macho kwa mara ya kwanza, akishangazwa na uumbaji wote uliomzunguka.


            Kwa muda mrefu, Mumba aliishi na Mtu, akimfundisha namna ya kulima, kutafuta chakula, na kujilinda dhidi ya hatari. Alimpa maarifa juu ya mimea ya dawa, wanyama, na majira ya mwaka. Mumba alimfundisha pia kuhusu upendo, uvumilivu, na maelewano ili Mtu aweze kuishi kwa amani na viumbe vingine vyote.


            Lakini Mumba alijua pia kwamba Mtu hakuwa peke yake; alihitaji mwenzi. Kwa hivyo, usiku mmoja, Mumba alipomweka Mtu katika usingizi mzito, alichukua ubavu mmoja kutoka mwilini mwake na kutoka humo akaumba kiumbe mwingine, mwanamke, na kumpa jina Hawa. Hawa alikuwa mrembo na mwenye hekima, akawa rafiki na msaidizi wa Mtu.


            Hapo ndipo walipoanza kuijaza dunia kwa watoto na wajukuu, wakisambaa kila kona ya ardhi, na kufurahia mazao ya dunia. Hadi leo, kizazi cha Mtu na Hawa kinaendelea, na wanaendelea kuishi kwa hekima na mafunzo ambayo walipokea kutoka kwa Mumba. Hadithi yangu inaishia hapo.