Namna ya kulezea mandhari

Mandhari Katika Fasihi

MAANA

Ni sehemu ambapo au mazingira ambako matukio ya hadithi au masimulizi yanafaanyika.

Kazi ya fasihi hujengwa katika mazingira maalum ambayo huitwa mandhari.

UFAFANUZI

  • Mandhari katika kazi ya fashi husaidia kuleta hisia iliyokusudiwa.
  • Mfano kama msanii anakusudia kuleta hisia ya woga humlazimu kuchukua mandhari ya woga kama msitu mnene, ngurumo za wanyama wakali.
  • Huonyesha jamii,mahali,wakati wa kihistoria na hali ya maisha ambambo mwandishi anaandika kazi yake.
  • Mandhari ya riwaya ni mapana na yanayoendelezwa kikamilifu kwa sababu riwaya hujihusisha na vipengele vingi vya maisha ambavyo hupatikana katika nyakati na mahali tofauti kama vile

shuleni,mijini,vijijini,ng’ambo….

  • Hali mbalimbali pia huweza kujitokeza.kwa mfano, hali ya huzuni, furaha,ufanisi,kupungukiwa,kufiwa…..
  • Mandhari husaidia kueleza maudhui na dhamira ya mwandishi.
  • Maudhui ya kazi lazima yelenge kipindi cha wakati ambapo kazi imeandikwa

Vipengele vya mandhari

  1. Wakati wa kutukia kwa matendo
  2. Kutambulisha wahusika.
  3. Kuonyesha migogoro.
  4. Kuonyesha matatizo ya kijamii- ulevi,ufisadi,wizi.
  5. Kueleza mahali pa tukio.
  6. Kuonyesha taharuki.
  • Kuonyesha maudhui
  • Kuonyesha hali- hali ya huzuni.
  • Kuonyesha kipindi cha wakati-wakati wa ukoloni
  • Kuonyesha utamaduni wa jamii
  • Kulinganua hali za matabaka.
  • Kuonyesha hali ya kiuchumi- je kuna mgao sawa wa mali

SWALI

“ Najihisi kama Kurwa katika novella ya Kurwa na Doto”

Eleza umuhimu wa nafsineni katika kufanikisha mandhari katika riwaya ya Chozi la Heri.

JIBU

  1. Mandhari huashiria mahali – kupitia mhusika umu tunaona anasomea shule ya tangamano pamoja na wanafunzi wenzake.
  2. Mandhari huashiria wakati – kupitia umu tunapata wasichana wanne bwenini wakielezana matatizo
  3. Mandhari huashiria wahusika – kupitia umu tunaona utepetevu wa askari kazini
  4. Mandhari huchimuza maudhui – kuptia umu tunapata maudhui ya changamoto za malezi anapoachwa na wanuna wake katika mlima wa simba
  5. Mandhari huibua taharuki – umu anatuonyesha kwao kulikuwa mlima wa simba babake alikozikwa hatujui kama waliwahi rudi huko tena
  6. Mandhari huonyesha hali – kupitia umu tunapata hali ya masikitiko wanayopitia wanafunzi pale shule ya Tangamano
  7. Mandhari huashiri tabaka – kupitia mandhari ya nyumbani mwa mwnageka anakopangwa umu kunaashiria tabaka la juu
Share this;

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *