Category Archives: Lessons

Alama za uakifishaji

Alama za uakifishaji hutumika katika maandishi ili kufafanua maana, kutenganisha mawazo, na kupanga sentensi. Zinasaidia wasomi kuelewa jinsi sentensi inavyopaswa kusomwa, kama ni swali, taarifa, au mshangao, na kutoa mapumziko au msisitizo inapohitajika. Baadhi ya alama za uakifishaji zinazotumiwa sana ni kama vile:

  1. Nukta (.)
  2. Koma (,)
  3. Kiulizi(?)
  4. Alama ya mshangao (!)
  5. Koloni (:)
  6. semikoloni (;)
  7. Alama za kunukuu (“ ”)
  8. kibainishi (’)
  9. Mabano ( )
  10. kistari kifupi (-)
  11. alama za dukuku (…)

Alama za uakifishaji zinasaidia kupanga maandishi na kuhakikisha kwamba maana inayokusudiwa inafikishwa wazi kwa msomi/msikilizaji.

Alama za mtajo/usemi (” ”)

a) Usemi Halisi
“Njoo kesho,” mama akamwambia.

b) Lugha Geni/Neno la Kukopwa

“Ninunulie ‘Indomie’ ukifikia sokoni.

c) Kuandika Anwani za Filamu,

“Vioja Mahakamani”


Nukta za Dukuduku (…):

a) Kuonyesha maneno yameachwa
Haraka haraka…

b) Kukatizwa usemi/kauli

Mama: Umesema…

Mtoto: Nimesema nitarudi jioni.


Koma/Mkato/Kipumuo (,):

a) Pumziko fupi katika sentensi
Je, utarudi leo?

b) Kuorodhesha
Alinunua mboga, samaki, nyanya, na viazi.


c)Katika Usemi Halisi

“Nitachelewa,” mama akamwambia.

d) Kuandika Anwani

Wizara ya Elimu,
S.L.P 10,
Naoirobi.

e) Kuandika Tarehe

Alibatizwa mwezi wa Julai, tarehe 20, 2007.


Ritifaa/Kibainishi (’):

a)Herufi imeachwa
Wal’otutuma

b)Shadda/Mkazo

‘iba, ka’lamu


c) Sauti ya King’ong’o

Ng`ombe amekufa.


Mshazari/Mkwaju (/):

a) Tarehe
Alizaliwa tarehe 5/6/1998.

b) Kuonyesha Kumbukumbu
KUMB 1/2024

c) Kuonyesha Visawe
Nenda katika shule/skuli.

d) Kuonyesha “Au”
Wazazi/walezi wamearikwa.


Kistari kifupi (-):

a)Kuandika Tarehe
5-6-2013

b)Kutenga Silabi
a-la-ye

c) Hadi/Kipindi cha Tukio Fulani
1999-2008

d) Kutenganisha Usemi na Msemaji
Lazima tufanye kazi kwa bidii-Kibaki


Kistari Kirefu (–):

a) Kutoa Maelezo Zaidi
Nchi za Afrika Mashariki – Kenyana Tanzania – zinatumia Kiswahili kama lugha ya kitaifa.

c) Kuonyesha Msemaji wa Kauli Fulani
Umoja ni nguvu – Nyerere.


Kikomo/Kitone/Nukta (.):

a) Mwisho wa Sentensi
Atafika kesho.

b) Kuandika Tarehe
12.5.2021

Kuonyesha Ufupisho wa Maneno
Dkt., Bw.,

Kutenga Shilingi na Senti
10.20 – Shilingi kumi na senti ishirini


Nusu/Semi Koloni/Nukta Mkato (;):

a) Kugawa Sentensi Bila Viunganishi
Amekulete zawadi nyingi; hazijakufurahisha.

Kama Kipumziko Katika Sentensi Ndefu
Baada ya kuchunguza hati aliyopewa na wafanyabiashara hao, aligundua haikuwa nzuri; hivyo akaamua kujiondoa nayo.


Vifungo/Mabano/Paradesi ( ):

a) Kuonyesha Maelezo ya Vitendo vya Msemaji/maleezo ya jukwaa
Fatuma: (Akicheka.) Umeshiba kweli!

b) Kutoa Maelezo Zaidi
Amin(alituzwa na rais) amepandishwa cheo.


Herufi Kubwa (H):

Mwanzoni mwa Sentensi
“Twendeni zetu,” akatwambia.

Baada ya alama hisi katika sentensi hisishi.

  • Salale! Umepoteza pesa zote.

Mwanzoni mwa Nomino za Pekee
Hadija, Kenya, Uganda, Jumamosi

Ufupisho wa Maneno
C.C.M (Chama cha Mapinduzi)


Koloni/Nukta Mbili (:)

a) Kuonyesha Orodha
Ili kuandaa samosa, unahitaji viungo vifuatavyo: unga, nyama, chumvi, mafuta, na kitunguu.

b) Kuandika Mazungumzo
Rhoda: Umekawia wapi?

c) Kutenganisha Saa na Dakika
7:45


Hisi/Mshangao (!):

Kuamrisha
Kachezeeni nje!

Baada ya Vihisishi
Masalaale! Pesa zangu zote zimeibwa.


Kiulizo (?):

Mwisho wa Sentensi ya ulizi
Umetoka wapi?


Herufi Nzito (h):

Kusisitiza
Jibu maswali manne pekee.


Herufi za Mlazo/Italiki (h):

Kuonyesha Neno la Kigeni
Tumealikwa na President.


Kinyota (*):

Kuonyesha neno fulani limeendelezwa Vibaya

Nipe shilingi *isirini.

Share this;

Domestic animals in Swahili

  1. Dog – Mbwa
  2. Cat – Paka
  3. Cow – Ng’ombe
  4. Sheep – Kondoo
  5. Goat – Mbuzi
  6. Pig – Nguruwe
  7. Chicken – Kuku
  8. Turkey – Bata mzinga
  9. Duck- bata bukini
  10. Horse – Farasi
  11. Donkey – Punda
  12. Camel – Ngamia
  13. Rabbit – Sungura
  14. Guinea fowl – kanga
  15. Parrot – Kasuku
Share this;

Numbers 1-100 in Kiswahili

  1. Moja
  2. Mbili
  3. Tatu
  4. Nne
  5. Tano
  6. Sita
  7. Saba
  8. Nane
  9. Tisa
  10. Kumi
  11. Kumi na moja
  12. Kumi na mbili
  13. Kumi na tatu
  14. Kumi na nne
  15. Kumi na tano
  16. Kumi na sita
  17. Kumi na saba
  18. Kumi na nane
  19. Kumi na tisa
  20. Ishirini
  21. Ishirini na moja
  22. Ishirini na mbili
  23. Ishirini na tatu
  24. Ishirini na nne
  25. Ishirini na tano
  26. Ishirini na sita
  27. Ishirini na saba
  28. Ishirini na nane
  29. Ishirini na tisa
  30. Thelathini
  31. Thelathini na moja
  32. Thelathini na mbili
  33. Thelathini na tatu
  34. Thelathini na nne
  35. Thelathini na tano
  36. Thelathini na sita
  37. Thelathini na saba
  38. Thelathini na nane
  39. Thelathini na tisa
  40. Arobaini
  41. Arobaini na moja
  42. Arobaini na mbili
  43. Arobaini na tatu
  44. Arobaini na nne
  45. Arobaini na tano
  46. Arobaini na sita
  47. Arobaini na saba
  48. Arobaini na nane
  49. Arobaini na tisa
  50. Hamsini
  51. Hamsini na moja
  52. Hamsini na mbili
  53. Hamsini na tatu
  54. Hamsini na nne
  55. Hamsini na tano
  56. Hamsini na sita
  57. Hamsini na saba
  58. Hamsini na nane
  59. Hamsini na tisa
  60. Sitini
  61. Sitini na moja
  62. Sitini na mbili
  63. Sitini na tatu
  64. Sitini na nne
  65. Sitini na tano
  66. Sitini na sita
  67. Sitini na saba
  68. Sitini na nane
  69. Sitini na tisa
  70. Sabini
  71. Sabini na moja
  72. Sabini na mbili
  73. Sabini na tatu
  74. Sabini na nne
  75. Sabini na tano
  76. Sabini na sita
  77. Sabini na saba
  78. Sabini na nane
  79. Sabini na tisa
  80. Themanini
  81. Themanini na moja
  82. Themanini na mbili
  83. Themanini na tatu
  84. Themanini na nne
  85. Themanini na tano
  86. Themanini na sita
  87. Themanini na saba
  88. Themanini na nane
  89. Themanini na tisa
  90. Tisini
  91. Tisini na moja
  92. Tisini na
  93. Tisini na tatu
  94. Tisini na nne
  95. Tisini na tano
  96. Tisini na sita
  97. Tisini na saba
  98. Tisini na nane
  99. Tisini na tisa
  100. Mia moja

Share this;