SHAMIRISHO
Shamirisho ni nomino ambayo huashiria kitendwa/mtendwa au kitendewa/mtendewa katika sentensi.
Nomino hii huweza kuambatana na kivumishi/vivimushi.
Aina za shamirisho
Kuna aina tatu za shamirisho
- Shamirisho kipozi/yambwa tendwa
- Shamirisho kitondo/yambwa tendewa/yambiwa
- Shamirisho ala
Shamirisho kipozi (direct object)
Ni nomino ambayo hupokea athari ya kitenzi moja kwa moja
Mifano;
- Mama anapika chakula.
- Mama anapika chakula kitamu
- Mama anapika chakula kitamu sana
Chakula/chakula kitamu/chakula kitamu sana ni shamirisho kipozi kwa sababu chakula kinatendwa/kinapokea kitendo moja kwa moja.
Mifano zaidi
- Nyumba kubwa iliyojengwa jana imebomoka.
- Anita alimkatia mtoto mkate kwa kisu.
- Mwanaheri alinunua simu yenye rangi nyingi.
Shamirisho kitondo (indirect object)
Ni nomino ambayo huathiriwa na kitendo kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
Sentensi nyingi huwa na vitenzi katika kauli ya kutendea/kutendewa.
Mfano
- Anita alimkatia mtoto mkate kwa kisu.( Nani alitendewa ? mtoto)
- Shangazi alimnunulia babu yangu koti. (Nani alitendewa? Babu yangu)
Shamirisho ala/kitumizi
Hii ni nomino ya kifaa ambacho hutumiwa kutendea kitendo fulani
Mara nyingi hujitokeza katika vielezi vya namna ala
Kihusishi “kwa” si sehemu ya shamirisho ala
Mfano
- Anita alimkatia mtoto mkate kwa kisu .(Alitumia nini kukata mkate? Kisu)
- Nyumba hiyo ilijengwa kwa mawe. (nyumba ilijengwa kwa kutumia nin? Mawe)
- Abiria watasafiri kwa basi kubwa. ( abiria watatumia nini? Basi kubwa)
Maswali
Bainisha shamirisho katika sentensi zifuatazo
- Alisema atamjengea mshindi nyumba ya mbao.
- Mgonjwa alitibiwa na daktari kwa dawa ghali.

The explanations were quite awesome …..??thanks so much be blessed
I hope this will help many students who didn’t understand the term shamirisho
Thank you
Thanks for the information it really helped
we need pple like u
Thank you
nice work
okay men
I like thi wark may God bless you people
thanks alot for the explanation
Type here..Thanks for helping me benefit am happy be blessed
Type here..thanks and good work
It’s really easy to understand. Thanks ?
Wow?Thank you so much for the help
nice work man
Thank you so much of helping to gain a lot on shamirisho and rest of student
Mbona nachanganyikiwa zaidi? Yambwa ni nomino mbona unaongeza kivumishi na kielezi hapo kwenye mifano yako?
Thanks alot???
Mungu azidi kuwabariki kwa kazi yenu na mzidi kupitisha mafuno kama haya katika mtandao ili tupate kuelewa kiswahili kwa upana.
Type here..amen
Type here..nice work
Kazi safi,maelezo yanayoeleweka kwa urahisi.
Thank you for you help men.I realy appreciate